BREAKING NEWS

[5]

NAMNA YA KUKUZA NA KUIMARISHA ROHO YAKO-3



KUSIFU NA KUABUDU

Tunaendelea na mwendelezo wa somo letu wa namna ya kukuza na kuimalisha roho yako, na sasa tunaingia jambo la pila baada ya kujifunza jambo la kwanza ambalo ni neno la Mungu.  Na sasa ni kusifu na kuabudu.
Kusifu na kuabudu ni njia nyingine ambayo unaweza kuitumia kukuza na kuimarisha roho yako. Mungu pia huitumia sana njia hii anapotaka kuimalisha roho yako. Ikumbukwe kwamba, kama nilivyosema hapo awali, njia zote hizi zinalenga kumkaribia Mungu, kwa sababu mtu anaimarika rohoni kwa kadiri anavyomkaribia Mungu. Uimara rohoni ni matokeo ya ukaribu na Mungu. Kusifu na kuabudu ni njia moja wapo iliyorahisi kumkaribia Mungu. Kwa sababu kuabudu kunahusisha roho (ya kwako) na Roho ya Mungu kushirikiana. Kuabudu ni kuileta roho yako kwenye makutano na Roho ya Mungu uweponi mwake.

Kabla ya kuendelea mbele zaidi ni vyema tukaelewa maana ya kusifu na kuabudu ili tuweze kuelewa ipasavyo namna ambavyo kunaweza kukuza na kuimarisha roho ya mtu. Kusifu na kuabudu ni maneno mawili tofauti yenye maana tofauti pia ingawa yanatumika pamoja. Utofauti wao unatokana na kitendo chenyewe na matokeo yake.

Uligeuza maombolezo yangu kuwa kucheza, ulinivua nguo za gunia ukanivika furaha, ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya. Ee BWANA wangu, nitakushukuru milele.” (Zab 30:11-12)



“Nitakushukuru milele kwa maana umetenda; Nitalingojea jina lako kwa kuwa ni jema; mbele ya wacha Mungu wako” (Zab 52:9)



“Haleluya, Enyi mataifa yote, msifuni BWANA, Enyi watu wote, mhimidini. Maana fadhili zake kwetu ni kuu, Na uaminifu wa BWANA ni wa milele” (Zab 117:1-2)



Ukiangalia mistari hii na mingine mingi kwenye biblia unaweza ukaelewa kiurahisi maana ya kusifu. Zaburi ya 30 inasema uligeuza maombolezo yangu kuwa kucheza ili moyo wangu ukusifu wewe, Zaburi ya 117 inasema enyi mataifa msifuni BWANA, kwa maana fadhiri zake ni za milele. Kwa hiyo kusifu ni matokeo ya kile ambacho Mungu amekifanya. Amegeuza maombolezo, amedhihirisha fadhiri zake, kwa sababu hiyo Mungu anasifiwa. Tunamsifu Mungu kwa matendo yake makuu aliyoyatenda na kuyafunua. Kwa ujumla tunaweza kusema;



Kusifu ni mwitikio wa moyo wa mtu kwa yale ambayo Mungu ameyatenda. Ni kukiri na kutangaza yale ambayo Mungu ameyafanya.



Mwitikio ni matokeo ya moyo kutambua (Recognize) yale ambayo Mungu ameyafanya iwe ni kwake au mtu mwingine. Sifa za Daudi, Asafu na wanawe, Yeduthuni na wanawe zilikuwa ni matokeo ya mambo ambayo Mungu alitenda kwao na katikati ya Israeli. Daudi anaposifu uweza wa Mungu kuokoa na mauti, ni kwa sababu aliona jinsi alivyomuokoa na mauti kutoka mkono wa Sauli na adui zake wengine. Hatusifu kwa sababu eti tunajisikia kufanya hivyo, hapana ila ni matokeo ya ufahamu ulioingia moyoni kwamba hakika kilichofanyika ni mkono wa Mungu kiasi ambacho moyo wake hauwezi kutulia. Daudi anasema,”….. ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya…..” Zab 30:11-12). Moyo unashindwa kutulia ni kwa sababu ya kutambua kile ambacho Mungu amekifanya mishani mwako au kwa watu wengine. Hatusifu kwa sababu tu tumeambiwa na kusikia tu bali kwa sababu mioyo yetu inatambua na kudhibitisha hayo matendo makuu ya Mungu. When our hearts realize what God has done, praises flow out of us. Unapoona mtu anapoambiwa huu ni mda wa kumsifu Mungu, tuwapo sehemu za ibada, lakini hajali, ni udhihirisho wa kwamba moyo wake hautambui mambo ambayo Mungu ameyafanya hata kama ameyasikia hayo.



Ndipo Yesu akaanza kuilaumu miji ambamo alifanya miujiza yake mingi kuliko kwingine, kwa maana watu wake hawakutubu.  “Ole wako, Korazini! Ole wako Bethsaida! Kwa maana kama miujiza iliyofanyika kwenu, ingelifanyika Tiro na Sidoni, miji hiyo ingekuwa imetubu tangu zamani kwa kuvaa magunia na kujipaka majivu”. (Math 11:20-21)



Miji ya korazini na Bethsaida ilikuwa ni baadhi ya miji iliyo kushuhudia matendo makuu ya Mungu kwa ishara na miujiza kupitia mwanae Yesu Kristo lakini mioyo yao isiweze kutambua. Their heart never recognized and realized God’s doings in their midist, and thus didn’t turn back to God. Realizing, everytime God does His work, it is a sign that you are spiritually alive. Most of the time when God does anything, He intends to awaken your spirit (heart)- bringing it to it’s original sense. Hiki ndicho alichokuwa anajaribu kufanya kwa miji ya korazini na Bethsaida, mioyo yao iweze kuamka na kutambua kinachofanyika ile iweze kumrudia Mungu.



Nazungumza kwa habari ya moyo (roho) wako. Kama moyo wako hauwezi kutambua kile ambacho Mungu amekifanya, kusifu kwako hakuna nguvu- your praises has no power, it loose it’s meaning. Mioyo yetu inapokosa ufahamu juu ya kile ambacho Mungu amefanya hata kama tumesikia, kusifu kwako kunakosa maana kwa sababu hiyo kunakosa nguvu. Kwa mfano, tunaposhindwa kutambua jinsi Mungu alivyomfufua Yesu toka kwa wafu kwa uweza wa Roho wake mtakatifu, hata kama tumesikia, sifa zetu hazina maana kwa sababu hiyo zinakosa nguvu. Kwa sababu hatuwezi kumsifu Mungu kwa maneno tu alafu mioyo yetu iko mbali. Daudi anasema. ,”….. ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya…..”. kusifu kunakuwa na maana na nguvu kunapokuwa ni matokeo ya moyo kushindwa kutulia kwa sababu ya kile ambacho Mungu amekifanya.



Basi Waisraeli walipoona uwezo mkubwa BWANA aliodhihirisha dhidi ya Wamisri, watu wakamwogopa BWANA na wakaweka tumaini lao kwake na kwa Musa mtumishi wake. Ndipo Musa na Waisraeli wakamwimbia BWANA wimbo huu: “Nitamwimbia BWANA, kwa kuwa ametukuka sana. Farasi na mpanda farasi amewatupa baharini. BWANA ni nguvu zangu na wimbo wangu, amekuwa wokovu wangu. Yeye ni Mungu wangu, nami nitamsifu, Mungu wa baba yangu, nami nitamtukuza. …..Na Miriamu, nabii mke, ndugu yake Haruni, akatwaa tari mkononi mwake na wanawake wote wakamfuata na matari yao wakicheza. Miriamu akawaitikia ‘‘Mwimbieni BWANA, kwa maana ametukuka sana. Farasi na mpanda farasi amewatupa baharini” (Kut 14:31, 15:1, 20-21)



Waisraeli walipoona uweza mkubwa ambao BWANA aliufanya katikati yao waliingiwa na hofu ya kumuheshimu Mungu- ile hofu ni uthibitisho ya kwamba mioyo yao imetambua na kukubali kile ambacho Mungu alikifanya kiasi ambacho walishindwa kujizuia, wakaanza kumwimbia Mungu kwa kuyakiri na kuyatangaza yale matendo makuu. Mioyo ilikuwa kama vile karibia inapasuka kiasi ambacho wanawake wa waisraeli walishindwa kujizuia. Miriamu pamoja na wanawake wote wakajipanga pamoja kwa matari na kuimba na kucheza. Why all the praises and the dances? Kwa sababu mioyo yao ilishindwa kutulia kwa kile ambacho Mungu amekifanya katikati yao. Kuimba na kucheza ilikuwa ni mwitikio wa roho zao. Kuimba na kucheza kunapokuwa ni mwitikio wa roho yako, hakuna kinachoweza kukuzuia. Hakuna sababu yoyote itakayoweza kukuzuia usimsifu na kumchezea Mungu. Maumivu, magonjwa, aibu, cheo n.k, vyote hivi haviwezi kukuzuia. Kwa sababu hiyo Mungu anakuwa kiini cha sifa zako.



Kwako wewe hutoka kiini cha sifa zangu katika kusanyiko kubwa, nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wakuchao wewe” (Zab 22:25)



Sipati picha jinsi ambavyo kanisa lingekuwa linalipuka kwa sifa na kucheza namna hii. Lakini kilicho kibaya zaidi ni kwamba mataifa wanaweza wakatambua matendo makuu mioyoni mwao kuliko hata watu wa Mungu, ndio maana hata mataifa wwanaweza kumsifu Mungu. Wakati waisraeli wanalalamika kwamba Musa amesabisha mateso yao yaongezeke, ni wakati huo huo waganga wanamwambia Farao hakika hiki ni chanda cha Mungu katika jambo ambalo Mungu alilifanya. Mungu alitazamia watu wake wangekuwa mstari wa mbele kuyatangaza matendo yake- ndiyo kuyatangaza, kwa sababu kusifu ni kuyatangaza na kuyakiri matendo makuu ya Mungu. Mtu anapokuwa kimya asifanye jambo lolote, hawezi kusifiwa lakini anapofanya jambo, hujidhirisha kwa watu, na sifa zake husambaa na kwenda mbali kwa kutangazwa na watu. Na Mungu hivyo hivyo anapojifunua kwa matendo yake, anatarajia watu wake wayakiri na kuyatangaza kwa mataifa ndio maana Daudi anasema,



Mwimbieni BWANA sifa, ametawazwa Sayuni, tangazeni miongoni mwa mataifa yale aliyoyatenda (Zab 9:11)



 Haleluya!

Kusifu kunamfanya Mungu aweze kuyaachilia yale mambo aliyoyakusudia maishani mwa mtu. Kusifu kunatngeza mazingira ya Mungu kuenda mahali pake kwa ajili yako na kufanya aachilie nguvu zake. Katika soma yangu biblia nikagungua Mungu huketi sehemu mbili tu, juu ya kiti chake cha enzi na juu ya sifa za watu wake. Kwa hiyo sifa zinageuzwa kuwa mahali pa kuketi pa Mungu. Kwa sababu sifa zinapotangazwa zinambeba Mungu kwa heshima yake ile ile. Ni muhimu kutangaza sifa za Mungu kwa ajili ya Mungu na kwa ajili yetu pia. Kwa Mungu jina lake linasambaa, na kwetu ni wokovu.



Kuabudu. Baada ya kuchambua kidogo kuhusu kusifu, ni vyema tunaangalia pia kuabudu. Kuabudu ni tofauti na kusifu kwa sababu kuabudu kupo kiundani sana kuliko kusifu (worship is more deeper that praise) kwa maana kwamba kuabudu inahusu Mungu ni nani na wewe ni nani (Worship is about who God is and who you are). Kuabudu inahitaji uelewa wa Mungu ni nani na wewe ni nani (worship requires understanding who God is and understanding who you are). Haihusiani na kitu ambacho Mungu amekifanya bali jinsi alivyo. Lakini wengi tunabubu Mungu tusiyemjua vizuri. Yesu alimtahadharisha yule mwanamke msamalia akisema



Ninyi Wasamaria mnaabudu msichokijua. Sisi Wayahudi tunamwabudu Mungu tunayemjua kwa sababu wokovu unatoka kwa Wayahudi” (Yoh 4:22)



Wasamalia walikuwa wanaabudu Mungu wasiyemjua lakini wayahudi walimwabudu Mungu waliyemjua. Ndivyo itupasavyo kumwabudu Mungu tunayemjua. Ndio maana Paulo aliamua kuwasaidia watu wa Athene walipokuwa wanaabudu Mungu wasiyemjua ili waweze kumjua.



Ndipo Paulo akasimama katikati ya Areopago akasema, “Enyi watu wa Athene! Ninaona kwamba katika kila jambo ninyi ni watu wa dini sana. Kwa kuwa nilipokuwa nikitembea mjini na kuangalia kwa bidii vitu vyenu vya kuabudiwa, niliona huko madhabahu moja iliyoandikwa: KWA MUNGU ASIYEJULIKANA. Basi sasa kile ambacho mmekuwa mkikiabudu kama kisichojulikana, ndicho ninachowahubiria” (Matendo 17:22-23)

Kuabudu kuna msingi katika kumjua na kuelewa Mungu ni nani, asili yake na tabia zake. Paulo akaamua kuwasaidia kuelewa na kupata ufahamu juu ya Mungu wasiyemjua, ili wasifanye makosa tena kuabudu Mungu wasiyemjua. Ebu tuangalie kwa pamoja mstari ambao utaweza kutusaidia vizuri kuelewa kuhusu kuabudu.

Lakini saa yaja, tena ipo, ambapo wale waabuduo halisi, watamwabudu Baba katika roho na kweli. Watu wanaoabudu namna hii, ndio Baba anawatafuta” (Yoh 4:23)

A time will come, however, indeed it is already here, when the true (genuine) worshipers will worship the Father in Spirit and in truth (reality), for the father is seeking just such people as these as His worshipers” (John 4:23 AMP)

Kuna mambo kadhaa tunayoyaona kwenye huu mstari:-

1.      1. Kuna waabuduo halisi na wasio halisi,

Tofauti ya waabuduo halisi (genuine) na wasio halisi inakuja wakati wa kuabudu- kuabudu katika roho na kweli. Roho hapa inazungumziwa habari ya roho yako, na kweli hapa, kwenye biblia ya tafsiri ya kiingereza imeweka kwenye mabano neno reality ikiwa na maana ya uhalisia. Kwa hiyo waabuduo halisi watamwabudu BABA kwa roho zao lakini katika uhalisia wa BABA jinsi alivyo. Sababu ya kumwabudu Mungu katika roho ni kwa sababu yeye ni Roho (Yoh 4:24). Ni vyema kuelewa kwamba Mungu anatafuta roho zinazoweza kumwabudu yeye katika uhalisia wake. Roho zetu zinapata kuujua uhalisia wa Mungu jinsi alivyo kwa njia ya ufunuo katika neno lake kupitia Roho wake mtakatifu. Ufunuo unaoupata ndio unaokusukuma kumwabudu Mungu. Sababu inayowafanya wazee Ishirini na nne, wenye uhai wane na malaika wamwabudu Mungu bila kukoma ni kwa sababu wanamuona Mungu kwa uhalisia wake wote bila kipimo, utukufu wake wote na enzi yake yote.

Pia kukizunguka hicho kiti cha enzi palikuwa na viti ishirini na vinne na juu ya hivyo viti walikuwa wameketi wazee ishirini na wanne, waliovaa majoho meupe, wakiwa na taji za dhahabu vichwani mwao. Kwenye kile kiti cha enzi palikuwa panatoka miali ya umeme wa radi, ngurumo na sauti za radi. Mbele ya hicho kiti cha enzi, palikuwa na taa saba zilizokuwa zinawaka. Hizi ndizo Roho saba za Mungu. Pia mbele ya hicho kiti cha enzi palikuwa na kile kilichoonekana kama bahari ya kioo, iliyokuwa angavu kama jiwe lisilo na rangi yo yote ling’aalo sana……Kila mmoja wa hawa viumbe wenye uhai wanne, alikuwa na mabawa sita na kujawa na macho pande zote, hadi chini ya mabawa. Usiku na mchana hawakuacha kusema: ‘‘Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, ni Bwana Mungu Mwenyezi, aliyekuwako, aliyeko na atakayekuja.’’ Kila mara viumbe hao wenye uhai wanne walipomtukuza, kumheshimu na kumshukuru Yeye aliyeketi kwenye kile kiti cha enzi, tena aishie milele na milele, wale wazee ishirini na wanne huanguka mbele Zake Yeye aliyeketi kwenye kile kiti cha enzi na kumwabudu Yeye aliye hai milele na milele. Wao huziweka taji zao mbele ya hicho kiti cha enzi wakisema” (Ufunuo 4:4-6, 8-10)



Hawa viumbe hai wanamuona na kukutana Mungu uso kwa uso mahali pale walipo. Wanapoona uzuri wa Mungu ulivyo, mngáo wa kiti cha enzi, na bahari ya kioo mbele za kiti cha enzi, ngurumo na radi zinazotoka hapo, zinawasukuma kumwabudu Mungu. Mungu anapojifunua, inatupa sababu ya kumwabudu. Na yeye hujifunua moyoni mwako. Yesu alimwambia mama msamalia kwamba watu hawataenda Yerusalemu kuabudu wala katika mlima, kwa maana huko ndiko Mungu alikuwa anajifunua lakini saa yaja ambayo ipo tayari ambayo Mungu atajifunua mioyoni mwa watu, na kwa sababu hiyo watamwabudu katika roho sawa sawa na ufunuo wanaoupata.  Mahali ulipo Mungu hujifunua moyo, ili uweze kumwabudu ndio maana akili wala mwili wako hauwezi kumwabudu Mungu.



Kuabudu ni kuingia katika uwepo wa Mungu kwa roho yako, mahali ambapo unakutana naye na kumwona alivyo. (Worship is about getting into God’s presence by your spirit, where you meet Him and experience His reality). Our spirits get to contact God who is Spirit in worship with a clear demarcation of who God is and who we are. In fact it is through worship we understand who we are. Kuabudu sio kuhusu nyimbo, kwa sababu unaweza ukamwabudu Mungu bila wimbo. Kuna wengine ambao wanalowea kwenye nyimbo na kuacha kiini cha kuabudu- Mungu mwenyewe. Na unaweza kufikia hapo kwa roho yako lasivyo haiwezekani hata kama ukiimba vizuri. Wakati wa kuabudu ndio wakati wa kukutana na nguvu za Mungu kwa sababu roho yako hukutana moja kwa moja na Roho ya Mungu- chanzo cha nguvu. Ndio wakati ambao tunapata nafasi ya kupokea vitu kutoka kwa Mungu ambaye ni Roho kwa roho zetu. Ni muda wa kujenga mahusiano mazuri na Mungu kwa sababu unapata nafasi ya kuutazama na kushiriki uhalisia na uzuri wake. Kwa sababu hiyo mtu hiimarika sana rohoni na kuwa na nguvu.



Endelea kufatilia mundelezo wa somo hili, Mungu akubariki
NAMNA YA KUKUZA NA KUIMARISHA ROHO YAKO-3 NAMNA YA KUKUZA NA KUIMARISHA ROHO YAKO-3 Reviewed by Unknown on 2:17:00 PM Rating: 5

No comments:

Sora Templates