BREAKING NEWS

[5]

SIFA KATIKA UZURI WA UTAKATIFU


2 Nyakati 20:21
"Naye alipokwisha kufanya shauri na watu, akawaweka wale watakaomwimbia BWANA, na kumsifu katika uzuri wa utakatifu...."


Duniani kunawaimbaji wazuri na wenye vipawa vikubwa sana na wanaonekana kumsifu Mungu vizuri. Kumwimbia na kumsifu Mungu sio jambo la mtu flani ila ni jambo la kila mmoja.
 
Watu wengi hatuoni baraka za Mungu zikishuka ktk maisha yetu ama Mungu akijidhihirisha uwepo wake wakati tunamwimbia na kumsifu kwa sababu tumekuwa tukimsifu vizuri ila hatujajua kumwimbia na kumsifu katika UZURI WA UTAKATIFU wake.... Hadi pale tutakapo ijua siri hii na kujifunza kumwimbia na kumsifu katika UZURI WA UTAKATIFU ndipo tutakapo muona Mungu akijidhihirisha!

Omba Roho Mtakatifu akufundishe jinsi ya kumsifu Mungu katika UZURI WA UTAKATIFU ili uzione baraka katika sifa.
 
Maandiko yanasema "....akawaweka wale watakaomwimbia BWANA, na kumsifu katika uzuri wa utakatifu..."
 
Mfalme hakuangalia nani anayejua kuimba na kumsifu Mungu maana naamini aliamini kuwa kila mtu anajua kumwimbia na kumsifu Mungu lakini alienda mbali zaidi i.e ili ashinde vita ni lazima awaweke watu wanaoijua siri iliyopo katika kusifu nao watamwimbia na kumsifu katika UZURI WA UTAKATIFU ili waweze kutangulia mbele ya jeshi kuhakikisha kuwa ushindi unapatikana kwa njia ya kumwimbia na kumsifu MUNGU kama alivyokuwa amewaambia.

Mungu akufundishe kumsifu YEYE maana ni zaidi ya kurukaruka, kukariri nyimbo na kutamka maneno.
SIFA KATIKA UZURI WA UTAKATIFU SIFA KATIKA UZURI WA UTAKATIFU Reviewed by RHEMA'S VOICE MINISTRY on 3:12:00 AM Rating: 5

No comments:

Sora Templates