NAMNA YA KUKUZA NA KUIMARISHA ROHO YAKO -1
“Yule
mtoto akakua, akaongezeka nguvu rohoni, akakaa majangwani hata siku ya kutokea
kwake kwa Israeli” (Luka 1:80)
“Yule
mtoto akakua, akaongezeka nguvu, amejaa hekima na neema ya Mungu ilikuwa juu
yake” (Luka 2:40)

“kama watoto wachanga waliozaliwa sasa
yatamanini maziwa ya akili yasiogoshiwa, ili kwa hayo mpata kuukulia wokovu”
(1Petro 2:2)
Ukisoma
mistari hii na mingine mingi katika biblia unaona wazi kwamba mtu anahitaji
kukua rohoni na kuongezeka nguvu kwa sababu anazaliwa akiwa mchanga rohoni
(immature). Mistari hii inatuonesha wazi kwamba mtu anatakiwa kukua sio tu
mwili bali na roho yake pia, kukua rohoni sio tu kwamba kunaongeza nguvu bali
kunaongeza hekima ndani ya mtu na neema juu yake. Mafanikio ya mtu yanategemea
sana mafanikio mazuri ya roho yake.
“Mpenzi naomba ufanikiwe katika
mambo yote na kuwa na afya yako, kama roho yako ifanikiwavyo”
(3 Yoh 1:2)
Hapo
tunaona wazi kwamba Mungu anataka tufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya lakini kwa kadiri ambavyo roho zetu
zinafaniwa. Kwa maneno mengine ni kwamba kiwango cha mafanikio ambacho mtu
anakifikia ni matokeo ya kiwango cha hali ya kiroho aliyoifikia. Kusudio la
Mungu ni tufanikiwe katika maeneo yote ya maisha sio tu machache, sio
unafanikiwa maswala ya kiuchumi halafu ndoa inakushinda, au unafanikiwa kielimu
halafu sehemu ya kazi unashindwa. Ukweli ni kwamba, roho ya mtu inapofanikiwa
katika eneo fulani, matokeo yake yanaonekana kwenye ulimwengu wa mwili kwenye
eneo hilo.
Kinachotakiwa ni kwamba mtu awe na ufahamu na nguvu za kutawala mazingira yake. Na kwa sababu ulimwengu wa mwili uliumbwa kutoka ulimwengu wa roho, kutawala mazingira ya ulimwengu wa mwili hainabudi kutawala ulimwengu wa roho kwanza ambao ndio unazaa mambo ya ulimwengu wa mwili. Ulimwengu wa roho maana yake ni eneo ambalo roho pekee ndizo zinazoenenda na kuishi huko. Ingawa roho yako iko ndani ya mwili lakini inaishi ulimwengu wa roho kwa hiyo mtu anaishi katika ulimwengu zote mbili kwa wakati mmoja. Mwili katika ulimwengu wa mwili na roho katika ulimwengu wa roho. Nafsi ndiye kiunganishi na mtafsiri kati ya roho na mwili. Kwa hiyo roho ya mtu inatakiwa iwe na ufahamu na nguvu ya kuutawala ulimwengu wa roho ili aweze kuutawala ulimwengu wa mwili. Kile ambacho unakiitaji (afya, ndoa, uchumi n.k) katika ulimwengu wa mwili inatakiwa roho yako iwe na nguvu ya kukifuata na kukiumba katika ulimwengu wa roho. Hii inakupa sababu ya kufikiri sana habari ya rohoni kuliko ya mwilini kwa sababu ya rohoni ndiyo yanayozaa ya mwilini.
Kinachotakiwa ni kwamba mtu awe na ufahamu na nguvu za kutawala mazingira yake. Na kwa sababu ulimwengu wa mwili uliumbwa kutoka ulimwengu wa roho, kutawala mazingira ya ulimwengu wa mwili hainabudi kutawala ulimwengu wa roho kwanza ambao ndio unazaa mambo ya ulimwengu wa mwili. Ulimwengu wa roho maana yake ni eneo ambalo roho pekee ndizo zinazoenenda na kuishi huko. Ingawa roho yako iko ndani ya mwili lakini inaishi ulimwengu wa roho kwa hiyo mtu anaishi katika ulimwengu zote mbili kwa wakati mmoja. Mwili katika ulimwengu wa mwili na roho katika ulimwengu wa roho. Nafsi ndiye kiunganishi na mtafsiri kati ya roho na mwili. Kwa hiyo roho ya mtu inatakiwa iwe na ufahamu na nguvu ya kuutawala ulimwengu wa roho ili aweze kuutawala ulimwengu wa mwili. Kile ambacho unakiitaji (afya, ndoa, uchumi n.k) katika ulimwengu wa mwili inatakiwa roho yako iwe na nguvu ya kukifuata na kukiumba katika ulimwengu wa roho. Hii inakupa sababu ya kufikiri sana habari ya rohoni kuliko ya mwilini kwa sababu ya rohoni ndiyo yanayozaa ya mwilini.
“Kwa kuwa ile nia ya mwili ni
mauti; bali nia ya roho ni uzima na amani” (Rumi 8:6)
Kufikiri
sana habari na mambo ya mwilini kunamfanya mtu mwili wake kuwa na nguvu na
kuyafanya hayo kuliko roho yake, ambao nia yake ni mauti. Lakini nia ya roho ni
uzima na amani, kwa hiyo ili uzima na amani vitokee, roho inatakiwa kuwa na
nguvu kuliko mwili. Mauti imezwe na uzima. Ili magonjwa yamezwe na uzima, roho
ya mtu haina budi kuwa na nguvu na kuwa imara kuliko mwili wake unaoumwa. Kuna
mambo ambayo mwanadamu hataweza kuyapata na kuyafurahia hata kama ni yake kwa
sababu tu ni mchanga kiroho (Galatia 4:1-2) na hana nguvu rohoni.
“Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata
sasa, Ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka”
(Math 11:12)
“Maana ufalme wa Mungu si kula na
kunywa, bali ni haki na amani na furaha katika Roho mtakatifu”
(Rumi 14:17)
Shetani hata ruhusu kirahisi upate haki, amani na furaha ingawa ni mambo ya ufalme wa Mungu (ufalme wenyewe) ambayo ni stahiki yako, lakini aliye na nguvu huvipata kwa nguvu, asiye na nguvu hawezi kuvipata hivyo. Somo hili linakuja kwako upate kiu ya kuongeza msuli katika roho ili uweze kuvipata vile ulivyokuwa unavikosa.
Shetani hata ruhusu kirahisi upate haki, amani na furaha ingawa ni mambo ya ufalme wa Mungu (ufalme wenyewe) ambayo ni stahiki yako, lakini aliye na nguvu huvipata kwa nguvu, asiye na nguvu hawezi kuvipata hivyo. Somo hili linakuja kwako upate kiu ya kuongeza msuli katika roho ili uweze kuvipata vile ulivyokuwa unavikosa.
Kuna
mambo manne ya msingi ambayo kila mtu atakaye kukua, kuimarika na kuongezeka
nguvu kiroho hana budi kuwa nayo na kuyafanya kwa sababu hayo ndiyo chanzo na
msingi wa kuimarika kiroho. Mambo hayo ni neno
la Mungu, maombi, kusifu na kuabudu, ushirika na watakatifu. Mambo haya yote yanalenga kufikia jambo
moja tu muhimu, kumkaribia Mungu zaidi. Mungu kuongezeka Ukuu moyoni.
Wakati fulani Yohana mbatizaji aliposikia habari za Yesu alisema maneno haya “Basi hii furaha yangu imetimia. Yeye hana budi KUZIDI, bali mimi kupungua” (Yoh 3:30). Hii inampasa kila mtu anayezaliwa mara ya pili kuona kwamba Mungu anatakiwa azidi moyoni. Ukiwa safarini kwa gari, kwa mbali mlima unaonekana ni mdogo lakini kadri unavyoukaribia ndivyo na ukubwa wake unaongezeka kwenye upeo wa macho. Kiuhalisia sio kwamba ule mlima unaongezeka ukubwa bali kwa sababu ya upeo wa macho ya mtu. Ndivyo ilivyo tunapofanya bidii kumkaribia Mungu. Ingawa Yeye ni Yeye Yule habadiliki, lakini Ukuu wake huongezeka ndani yetu kwa kadiri tunavyozidi kuwa karibu naye.
Hapa nitakuwa nachambua jambo moja baada ya jingene kwa undani ili kuona ni namna gani kila moja linasaidia kukuza na kuimarisha roho yako.
Wakati fulani Yohana mbatizaji aliposikia habari za Yesu alisema maneno haya “Basi hii furaha yangu imetimia. Yeye hana budi KUZIDI, bali mimi kupungua” (Yoh 3:30). Hii inampasa kila mtu anayezaliwa mara ya pili kuona kwamba Mungu anatakiwa azidi moyoni. Ukiwa safarini kwa gari, kwa mbali mlima unaonekana ni mdogo lakini kadri unavyoukaribia ndivyo na ukubwa wake unaongezeka kwenye upeo wa macho. Kiuhalisia sio kwamba ule mlima unaongezeka ukubwa bali kwa sababu ya upeo wa macho ya mtu. Ndivyo ilivyo tunapofanya bidii kumkaribia Mungu. Ingawa Yeye ni Yeye Yule habadiliki, lakini Ukuu wake huongezeka ndani yetu kwa kadiri tunavyozidi kuwa karibu naye.
Hapa nitakuwa nachambua jambo moja baada ya jingene kwa undani ili kuona ni namna gani kila moja linasaidia kukuza na kuimarisha roho yako.
NENO
LA MUNGU
Ili
kuelewa neno la Mungu vizuri na jinsi linavyofanya kazi katika kukuza na
kuimarisha roho ya mtu, kuna mambo kadha wa kadha ambayo ni ya muhimu na msingi kuyafahamu na kuyafunga katika nia za viuno vyetu. Mambo hayo ni kama
ifuatavyo:-
Jambo
la kwanza
Neno ni Mungu mwenyewe.
Hili ni jambo la msingi kulifahamu na kulishika kwa kila mtu anayetaka
kufanikiwa kiroho kwa sababu linajenga picha halisi ya neno la Mungu.
“Hapo mwanzo, alikuwako Neno. Huyo Neno
alikuwa pamoja na Mungu, naye Neno alikuwa Mungu” (Yoh 1:1)
“Kisha nikaona mbingu imefunguka na hapo
mbele yangu akiwepo farasi mweupe, ambaye Yeye aliyempanda huyo farasi aliitwa
Mwaminifu na wa Kweli. Yeye ahukumu kwa haki na kupigana vita. Macho yake ni
kama miali ya moto na juu ya kichwa Chake kuna taji nyingi. Alikuwa na jina
lililoandikwa ambalo hakuna mtu ye yote anayelijua isipokuwa Yeye mwenyewe.
Alikuwa amevaa vazi lililochovywa kwenye damu na Jina lake ni ‘‘Neno la Mungu.’’ (Ufunuo 19:11-13)
Mistari
hii miwili inamuelezea Mungu kama neno kwa wazi zaidi. Yoh 1:1 inaeleza kwamba NENO
ndilo lililokuwapo tangu mwanzo na yeye NENO ndiye Mungu. Na Ufunuo 19:11-13
inaeleza kwamba kuna jina limeandikwa. Mistari hii yote miwili inaweka wazi kwamba
YESU ndiye NENO na ndiye Mungu. Hii inasadia kujenga imani na msimamo ndani ya moyo wa mtu
kwamba, kila unaposoma neno na kulitafakari, unasoma na kumtafakari Mungu
mwenyewe. Pale mwanzo nilisema njia zote tano za kukuza na kuimarisha roho yako
zinalenga katika kumkaribia Mungu na kuongezeka ndani, kwa hiyo yeye huongezeka
kwa kadiri unapomsoma na kumtafakari katika neno ambalo ndiyo yeye Mwenye.
Jambo
la Pili
Neno
ni Roho
Ieleweke
wazi kwamba neno ni Roho ikiwa na maana ya Roho mtakatifu lakini pia ikiwa na
maana ya kwamba linamakao katika ulimwengu wa roho. Kuna wakati fulani Yesu
alipokuwa akiongea na mafarisayo na masadukayo, walishindwa kumwelewa akiwa
anajizungumzia yeye kama mkate wa uzima na wanafunzi wake pia hawakumwelewa
ikabidi wamuulize, Yesu akajibu kwamba “Roho ndiye atiaye uzima,
mwili haufai kitu. Maneno haya niliyowaambia
ni Roho tena ni uzima” (Yoh 6:63). Paulo pia aliandika kwamba “Yeye
ndiye aliyetutosheleza kuwa wahudumu wa
agano jipya, si wa andiko bali wa roho, kwa maana andiko huua bali Roho
huhuisha (hutia uzima)” (2Kor 3:6)
Kuelewa kwamba neno ni roho ni Muhimu sana. Inakupa kuelewa kwamba unapolipokea neno hulipokei na kuliweka mwilini bali rohoni ili kuleta matokea katika mwili. Ukweli ni kwamba hakuna kitu chochote kinachoweza kufanyika mwili isipokuwa roho. Biblia inaposema kwamba “Naye Neno alifanyika mwili….” (Yoh 1:14) ina maana kwamba Neno ambaye ndiye Mungu ambaye ndiye Roho ndiye ambaye alifanyika mwili. Kwa sababu “…..’Bwana' ndiye Roho…”(2 kor 3:17).
Kuelewa kwamba neno ni roho ni Muhimu sana. Inakupa kuelewa kwamba unapolipokea neno hulipokei na kuliweka mwilini bali rohoni ili kuleta matokea katika mwili. Ukweli ni kwamba hakuna kitu chochote kinachoweza kufanyika mwili isipokuwa roho. Biblia inaposema kwamba “Naye Neno alifanyika mwili….” (Yoh 1:14) ina maana kwamba Neno ambaye ndiye Mungu ambaye ndiye Roho ndiye ambaye alifanyika mwili. Kwa sababu “…..’Bwana' ndiye Roho…”(2 kor 3:17).
Uzima
uko ndani ya roho. Uzima wa kitu chochote uko ndani ya roho yake hiyo kitu. Ili
hicho kitu kiihuike kinahitaji uzima ndani ya roho yake. Na roho iliyo na uzima
imefichwa ndani ya neno. Na neno linapotamkwa linahuisha ile roho iliyo na huo
uzima. Mungu anapotaka kuhuisha roho yako kwa uzima wake anakupa neno lake
lililo na roho ya uzima ndani yake, mchawi naye anapokutamkia maneno ya mauti,
roho ya mauti inahuika ndani na kutenda kazi.
Mambo
haya mawili yanatuwekea msingi kuelewa ni namna gani basi neno la Mungu
linavyoweza kuimarisha roho ya mtu. Mtu ni roho, anayo nafsi na anaishi kwenye
nyumba inayoitwa mwili. Kilicho muhimu ni roho kuliko vingine vyote, bali ili
roho iweze kufanya kazi vizuri hapa duniani inahitaji mwili na nafsi kama
mtafsiri kati ya mwili na roho. Roho inapaswa kushibishwa na mambo ya rohoni na
mwili kula vya mwilini. Kwa maana asili ya roho ni roho na asili ya mwili ni
udongoni.
Asante na Mungu akubariki. Endelea kufuatilia muendelezo wa somo hili.
NAMNA YA KUKUZA NA KUIMARISHA ROHO YAKO -1
Reviewed by Unknown
on
1:36:00 PM
Rating:

No comments: