KUTEMBEA KATIKA ROHO-2

KUTEMBEA KATIKA ROHO-2
Bwana Yesu asifiwe sana mwana wa
Mungu..!!
Karibu sana tuendelee na sehemu
ya pili ya Mwendelezo wa somo letu la KUTEMBEA KATIKA ROHO,kama hukupata nafasi
ya kupitia sehemu ya kwanza,unaweza kulipata kwenye blog yetu ya
rhemavoice.blogspot.com au kwenye page yetu ya facebook-Rhema’s Voice Ministry.
Sehemu ya kwanza tulishia kwenye
kuona Tabia za Roho Mtakatifu na Karama za Roho Mtakatifu.Leo tuanzia hapo hapo
kwenye tabia za Roho Mtakatifu.
Tabia ya Roho Mtakatifu ni ya
msingi sana kuliko Karama kwasababu kutembea kwako kwenye karama kutatunzwa na
tabia za Roho Mtakatifu ndani yako.Karama haiwezi kukulinda na dhambi bali
Tunda la Roho Mtakatifu.Ukifanikiwa kuwa na Karama kubwa halafu hujafanikiwa
kutembea katika matunda ya Roho Mtakatifu kuna hatari kubwa hiyo karama ikawa
chanzo cha anguko lako.Si maanishi kuwa Karama sio kitu cha msingi la hasha,ni
Kitu cha msingi ni kitendea kazi unachokihitaji ili uweze kusimama kwenye ofisi
uliyoitwa,lakini Tabia,Tabia ndio itakayokulinda,ndiyo itakayokupeleka mbali
katika safari ya Ofisi yako.
Tuangalie baadhi ya Watumishi wa
Mungu waliokuwa wakubwa sana kwenye Biblia,waliokuwa na Karama nyingi na za
kutisha lakini kwasababu ya kushindwa kutembea kwenye tabia za Roho Mtakatifu
kuna viwango hawakufikia,kuna mashambulizi walipata kutoka kwa adui na hata
wengine kuwa na mwisho mbaya.
Musa
Musa ni moja ya watumsh wakubwa
sana waliowahi kutembea na Mungu na kutembea katika uweza wa ajabu wa Roho
Mtakatifu.
Lakini pamoja na yote kuna
kiwango Musa hakufikia,alipaswa kufika Kaanani lakini hakuingia na ukichinguza
maandiko utakuja kuona kuwa Kushindwa kutembea katika Tabia/tunda la Roho
Mtakatifu ndio iliyomgharimu.
Hesabu 20:2-12
2 Na hapo hapakuwa na maji kwa ule
mkutano; wakajikusanya juu ya Musa na juu ya Haruni.
3 Watu wakashindana na Musa,
wakanena, wakisema, Ingalikuwa heri kama tungalikufa wakati ule ndugu zetu
walipokufa mbele za Bwana!
4 Mbona mmewaleta kusanyiko la
Bwana hata jangwa hili ili tufe huku, sisi na wanyama wetu?
5 Na mbona mmetupandisha kutoka
Misri ili kutuleta hata mahali hapa pabaya? Si mahali pa mbegu, wala tini, wala
mizabibu, wala makomamanga; wala hapana maji ya kunywa.
6 Musa na Haruni wakatoka pale
palipokuwa mkutano, wakaenda hata mlangoni pa hema ya kukutania, wakaanguka
kifudifudi; utukufu wa Bwana ukawatokea.
7 Bwana akasema na Musa, akinena,
8 Twaa ile fimbo, ukawakusanye
mkutano, wewe na Haruni ndugu yako, ukauambie mwamba mbele ya macho yao utoe
maji yake, nawe utawatokezea maji katika mwamba, na hivyo utawanywesha maji
mkutano na wanyama wao.
9 Musa akaitwaa hiyo fimbo kutoka
mbele za Bwana kama alivyomwamuru.
10 Musa na Haruni wakawakusanya
kusanyiko mbele ya mwamba, akawaambia, Sikieni sasa, enyi waasi; je!
Tuwatokezee maji katika mwamba huu?
11 Musa akainua mkono wake akaupiga
ule mwamba kwa fimbo yake mara mbili; maji yakatoka mengi, mkutano wakanywa na
wanyama wao pia.
12 Bwana akamwambia Musa na Haruni,
Kwa kuwa hamkuniamini mimi, ili kunistahi mbele ya macho ya wana wa Israeli,
basi kwa sababu hiyo, hamtawaingiza kusanyiko hili katika ile nchi niliyowapa.
Ukisoma maandiko haya utaona
jinsi kusanyiko lilivyomshambulia Mtmsh wa Mungu Musa hata kusababisha ashindwe
kufuata maelekezo aliyopewa na Mungu.Kwenye Mstari wa 12 Utaona Mungu akisema
Musa na Haruni hawakumwamini kwa kutokufuata maelekezo yake. Lakini ukienda
kwenye Zaburi utagundua kulikuwa kuna kitu zaidi kilichomfanya Musa akatenda
vile mbele za Bwana na kupewa adhabu ya kutokufika Kaanani.
Tazama haya maneno ya Musa kwa
umakini kuna kitu utakiona ndani ya Musa.
……Sikieni sasa, enyi waasi;
je! Tuwatokezee maji katika mwamba huu?
11 Musa akainua mkono wake akaupiga
ule mwamba kwa fimbo yake mara mbili; maji yakatoka mengi, mkutano wakanywa na
wanyama wao pia.
Utaona ndani ya haya Maneno ya
Musa kulikuwa kuna hasira ndani yake.Kutokana jinsi hawa jamaa walivyomsumbua
nafsi yake.
Zaburi 106:32-33
32 Wakamghadhibisha penye maji ya
Meriba, Hasara ikampata Musa kwa ajili yao,
33 Kwa sababu waliiasi roho yake,
Akasema yasiyofaa kwa midomo yake.
Ukisoma kwenye biblia ya
kingereza huu mstari wa 33 unasomeka hivi
Because they provoked his spirit,
so that he spake unadvisedly with his lips.(KJV)
They made him bitter so that he
spoke recklessly.(NSB)
Utaona hapa Musa alikasirishwa
sana nay ale manung’uniko ya Wanaisrael na matokeo
yake katika hasira alisema yasiyofaa na gharama yake ilikuwa kubwa sana.
Hasira ndiyo
iiyomgharimu,Palipohitajika Tunda la Uvumilivu hasira ikatawala ndani yake.
Utaona kuwa Karama alikuwa nayo ya Miujiza ya Ajabu lakani hakushughulikia
hasira yake na ilimgharimu.Hasira ya haraka,ya kulipuka,isiyoweza kutawaliwa ni
tunda la mwili ambalo kama hujachukua hatua kulishulikia litakukwamisha maeneno
mengi sana katika Kutembea kwako na Mungu.
Ukichunguza kwa makini utagungua
hasira ya Musa haikuwa hasira ya kawaida tu,ilikuwa ni hasira ya Laana.
Musa ni mwana wa Lawi,na Hasira
ya Baba yake Lawi ililaaniwa na Babu yao Mzee Yakobo.Kwa hiyo kulikuwa mlango
wa adui kupita na kumvuruga Musa kupitia Hasira.
Mwanzo 49:5-7
5 Simeoni na Lawi ni ndugu; Panga
zao ni silaha za jeuri.
6 Nafsi yangu, usiingie katika
siri yao, Fahari yangu usiungane na kusanyiko lao, Maana katika ghadhabu yao
walimuua mtu, Na kwa ukaidi wao walikata mshipa wa ng'ombe;
7 Ghadhabu yao na ilaaniwe, maana
ilikuwa kali, Na hasira yao, maana ilikuwa haina huruma. Nitawagawa katika
Yakobo, Nitawatawanya katika Israeli.
Sasa unaweza kuona chimbuko la
ile Hasira ya Musa.Kuna watu wana hasira za kawaida na kunawengine ni roho,inasukumwa
na nguvu ya giza ndani yake.Kwa Musa ilikuwa laana.Kuna watu wanahasira za
Kurithi,kwenye nyumba za Baba zao hasira kali ndio asili yao.Kitu kama hii bila
kuishughulikia kwa Msaada wa Roho Mtakatifu itakuharibia mambo mengi.
Mithali 16;32
Asiye mwepesi wa hasira ni mwema kuliko
shujaa; Na mtu aitawalaye roho yake kuliko mtu atekaye mji.
Hasira ni tabia ya Mungu ndani ya
mtu,lakini Mungu sio mwepesi wa hasira.Hivyo wana wake wanapaswa kutokuwa
Wepese wa Hasira.Unapaswa kuwa na uwezo wa Kuitawala hasira yako Mwana wa
Mungu.Huwezi kuwa Shujaa kama hujui kuitawala hasira yako.
Kutoka 34;6
6 Bwana akapita mbele yake,
akatangaza, Bwana, Bwana, Mungu mwingi wa huruma, mwenye fadhili, si mwepesi wa
hasira, mwingi wa rehema na kweli;
Yakobo 1;19
Hayo mnajua, ndugu zangu wapenzi.
Basi kila mtu na awe mwepesi wa kusikia, bali si
mwepesi wa kusema; wala
kukasirika;
Unaweza kujitetea ndivyo nilivyo
na utaendelea kubaki hivyo mpaka utakapokubali kuwa hiyo hasira ya haraka hivyo
sio Tunda la Roho Mtakatifu bali tunda la mwili na hapo utaanza kushirikiana na
Roho Mtakatifu katika kuitawala hasira yako ili isikuletee madhara maana ni
hakika itaharibu nafsi yako,mahusiano yako na watu na hata kutembea kwako
katika Karama za Roho Mtakatifu.
Jipime Yakobo anasema mpole wa
kunena na kukasirika bali mwepesi wa kusikiliza,ndivyo ilivyokwako au kwako
utaratibu umegeuka,yaani wewe ni mwepesi wa kukasirika na kuongea na sio
mwepesi kusikiliza.Upole ni Tunda la Roho,Uvumilivu ni Tunda la Roho kutembea
katika hayo ni kutembea katika Roho Mtakatifu.Kusudia kukua katika Uvumilivu na
Upole.
Kwa leo tuishie hapo mtu wa
Mungu,tutaendelea kwa kadiri Mungu atakavyotupa Neema yake.
Barikiwa
sana kwa Jina la Yesu Kristo
KUTEMBEA KATIKA ROHO-2
Reviewed by Unknown
on
8:18:00 PM
Rating:

No comments: