NAMNA YA KUKUZA NA KUIMARISHA ROHO YAKO-2
NAMNA YA KUKUZA NA KUIMARISHA ROHO
YAKO-2
Karibu
tuendelee na mfululizo wa somo hili la namna ya kuikuza roho yako na
kuimarisha. Naamini Mungu amekusudia ujifunze hili somo pamoja nasi ndio maana
ukapitia blogu hii. Roho mtakatifu aendelee kukufundisha unapoendelea kusoma na
kujifunza.
Tuliishia
sehemu kwamba,
Roho
inapaswa kushibishwa na mambo ya rohoni na mwili kula vya mwilini. Kwa maana
asili ya roho ni roho (Mungu) na asili ya mwili ni udongoni.
Roho
ya mtu iliumbwa wa neno la Mungu kutoka kwa Mungu. Vitu vyote pia viliundwa kwa
neno la Mungu. Ingawa vitu vyote vilitokea kwa neno kutoka kwa Mungu lakini
vilitokea kwa mwelekeo tofauti uliotengeneza asili kutofautiana.
“Kisha Mungu akasema, “Ardhi na itoe majani; miche itoayo mbegu,
miti juu ya nchi itoayo matunda yenye mbegu ndani yake, kila mmea kulingana na
aina zake mbalimbali.” Ikawa hivyo. Ardhi ikachipua mimea: Mimea itoayo mbegu
kulingana na aina zake na miti itoayo matunda yenye mbegu kulingana na aina zake.
Mungu akaona ya kuwa hili ni jema,,,, Mungu akasema “Kuwepo na viumbe hai tele
kwenye maji, ndege waruke juu ya dunia katika nafasi ya anga.’’ Kwa hiyo Mungu
akaumba viumbe wakubwa wa baharini na kila kiumbe hai kiendacho majini,
kulingana na aina zake na kila ndege mwenye mabawa kulingana na aina yake.
Mungu akaona kuwa hili ni jema. Mungu akavibariki akasema, “Zaeni mkaongezeke
mkayajaze maji ya bahari, nao ndege waongezeke katika dunia.’’ Ikawa jioni,
ikawa asubuhi, siku ya tano. Mungu akasema, “Ardhi na itoe viumbe hai kulingana
na aina zake: Wanyama wa kufugwa, viumbe vitambaavyo ardhini na wanyama pori,
kila mnyama kulingana na aina yake.’’ Ikawa hivyo. Mungu akafanya wanyama pori
kulingana na aina zake, wanyama wafugwao kulingana na aina zake na viumbe vyote
vitambaavyo juu ya ardhi kulingana na aina zake. Mungu akaona kuwa hili ni
jema” (Mwanzo
1:11-12, 20-25)
Ukisoma
mistari hii utagundua kwamba ingawa kote Mungu alitamka neno lakini alitamka
kwenda sehemu tofauti ambayo ndiyo inatuonesha kwamba kitu kilichoumbwa
kimeundwa na nini na kimetokea wapi. Mimea, miche na miti ilitokea katika
ardhi, samaki katika maji, wanyama wa kila aina kutoka katika ardhi. Alipotamka
kwenda kwenye ardhi, ardhi ikatoa hivyo viumbe, maji yakatoa samaki. Kwa hiyo
ingawa viumbe viliumbwa kwa neno la Mungu lakini vina asili ya udongo na maji
na ili viweze kustawi vinahitaji udongo na maji na vitu vilivyo na asili yao.
Miti, na wanyama inahitaji udongo, samaki wanahitaji maji kuishi.
Mungu
alipokuwa anamuumba mwanadamu, alisema neno kama alivyofanya kwa miti, miche,
samaki na wanyama lakini kwa mwelekeo tofauti. Wakati huu hakutamka kwenda
kwenye ardhi wala maji bali kwenda kwake mwenye na kutoka kwake mwanadamu
akatokea.
“Ndipo Mungu akasema, “Tufanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu,
wakatawale juu ya samaki wa baharini na ndege wa angani, juu ya mifugo, juu ya
dunia yote, na juu ya viumbe wote watambaao juu ya nchi.’’ Kwa hiyo Mungu
alimwumba mtu kwa mfano wake mwenyewe, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanaume
na mwanamke aliwaumba” Mwanzo 1:26-27.
Kama
vile neno la Mungu lilivyoenda katika ardhi, na ardhi ikatoa viumbe hai ndivyo
hivyo hivyo lilivyoenda kwa Mungu na Mungua akatoa mwanadamu. Kwa hiyo kama
vile mimea na wanyama ilivyo na asili ya udongo (ardhi) ndivyo hivyo hivyo
mwanadamu alivyo na asili ya Mungu. Ndiyo maana wanyama na mimea inapokufa
inarudi udongoni na mwanadamu akitoka duniani (kufa) anarudi kwa Mungu. Mungu
ni Roho (Yoh 4:24) ndiyo maana mwanadamu pia roho iliyo na asili ya Mungu.
Ndiyo maana mtu hatakiwi kujidharau hata kama wenzake wanamdharau kwa sabubu
ameundwa na vitu alivyoundwa navyo Mungu. Haleluya!
“BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi akampulizia pumzi ya
uhai puani mwake, mtu akawa nafsi hai” (Mwanzo 2:7)
Mstari
huu unatuonyesha mahali mwili wa mwanadamu ambao ndiyo nyumba ya roho yake
ulikotokea. Mungu alifanya mwili kutoka katika mavumbi ya ardhi, kwa maneno
mengine ni kwamba asili ya mwili ni mavumbi ya ardhi (udongo). Ndiyo maana mtu
anapouacha mwili, mwili hubadilika kuwa udongo katika asili yake. Mungu
alimwambia Adamu “Kwa
jasho la uso wako utakula chakula hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo
ulitwaliwa, kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi’’
(Mwanzo 3:19)
Ili
mwili uendelee kuwa na nguvu na kuishi vizuri kwa afya unahitaji kushibishwa na
vitu vya asili yake yaana ardhi (udongo). Mungu angali akijua hili alimwambia
mwanadamu
“Kisha Mungu akasema, “Nimewapa kila mche utoao mbegu juu ya uso wa
dunia yote na kila mti wenye matunda yenye mbegu ndani yake. Vitakuwa kwa ajili
ya chakula chenu, Cha wanyama wote wa dunia, ndege wote wa angani na viumbe
vyote viendavyo juu ya ardhi. Kila kiumbe chenye pumzi ya uhai, ninawapa kila
mche wa kijani kuwa chakula.’’ Ikawa hivyo” (Mwanzo 1:29-30)
Ili
kuhakikisha mwili unastawi na kunawili, Mungu akamwekea tayari mwanadamu vitu
hivyo ili aishi kwa hivyo. Mtu asipokula kwa mda mrefu mwili wake hudhoofika,
hukosa nguvu na hatimaye hufa kabisa. Na roho ya mtu ni hivyo hivyo pia. Sasa
kilicho muhimu kwa Mungu sio mwili bali roho ya mtu. Kama Mungu anajali mwili
wa mwanadamu namna hii si zaidi sana roho yake? Kwa sababu hii, akaweka tayari
pia chakula ambacho roho itashiba, kukua, kuongezeka nguvu na kustawi kwa hicho-
Neno lake- ambalo linaasili sawa na roho.
Mwili
hauwezi kula vitu vya rohoni bali unaweza kuhuishwa na roho yako. Uhai ulio
katika roho yako unaambukizwa katika mwili wako, roho yako inapopona na mwili
wako unapona. Na roho haiwezi kushibishwa na vitu vya mwilini kwa sababu vina
asili tofauti. Na mtu wa asili ya mwilini hawezi kupokea mambo ya rohoni (kwake
ni upuuzi) lakini mtu wa rohoni huvipokea.
Kwa
hiyo roho ya mtu inahitaji neno la Mungu (hicho ni chakula chake) kama vile
mwili unavyohitaji chakula chake (wali, ugali, mihogo, pizza, nyama n.k). Hilo
neno la Mungu linaenda kuimarisha roho ya mtu ndani na kumjengea msingi imara
ndani yake. Litakiwalo ni kwamba mtu inampasa kusoma neno na kulitafari. Ukila
wali baada ya mda unamengenywa na kufyonzwa na kuwa sehemu ya mwili.
Ukichunguzwa tumboni hawataona wali tena wala hawataweza kutofautisha kati ya
chakula ulichokula na mwili wako. Neno linatakiwa liwe sehemu ya roho yako pia.
Unapalitafakari neno sana lile neno linakuwa sehemu ya roho yako.
“Kwa maana Neno la Mungu li hai tena lina nguvu tena lina makali
kuliko upanga uwao wote wenye makali kuwili, tena linachoma hata kuzigawanya
nafsi na roho, viungo na mafuta yaliyo ndani yake, tena li jepesi kuyatambua
mawazo na makusudi ya moyo. Wala hakuna kiumbe chochote kilichofichika machoni
pa Mungu. Kila kitu kimefunuliwa na kiko wazi machoni pake Yeye ambaye Kwake
tutatoa hesabu”
(Ebrania 4:12-13)
Neno la Mungu ndilo liletalo uhai na nguvu
ndani ya roho ya mtu na kila wakati mtu huyo akilitafari neno hilo anapata uhai
mpya (kuhuishwa) na nguvu mpya. Kwa hiyo nguvu huongezeka rohoni kwa kadiri ya
kutafakari neno. Ni Neno la Mungu linalofungua masikio ya ndani (rohoni) ili
uweze kusikia vizuri kwa maana “…… kusikia huja kwa
neno la kristo” (Warumi 10:17)
Ukweli
ni kwamba tunaishi kwenye dunia ambayo inatufanya tuwe kwenye vita vya mara kwa
mara bila kupumzika (constant battle) na shetani. Sababu ni kwamba, mara tu mtu
anapozaliwa mara ya pili, ingawa anaisha ndani yake (dunia) lakini siyo sehemu
yake na anawekewa ndani yake namna ya kuibadiri dunia kwa ufalme wa Mungu. (to
effect the earth with the kingdom of God). Kwa hiyo mtu anatakiwa kuwa na
mfumo, sheria, taratibu, maagizo na amri tayari ndani yake na nguvu ya kupigana
ili kuyadhihirisha hayo. Neno la Mungu ndilo linalotengeza mfumo, sheria,
taratibu, maagizo na amri na nguvu inatokea ndani yake.
“ndivyo litakavyokuwa
neno langu, litokalo katika kinywa changu; halitanirudia bure, bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma” (Isaya 55:11)
Tafsiri
nyingine ya biblia imeandika hivi;
“ndivyo lilivyo neno langu lile litokalo kinywani mwangu:
Halitanirudia tupu, bali litatimiliza lile
nililokusudia na litafanikiwa katika
kusudi lile nililolituma”. (Isaya 55:11)
Biblia
inasema neno la Mungu lina nguvu, hiyo nguvu ndiyo inayofanya kutimizwa kwa
kile kinachosemwa na hilo neno. Kwa maneno mengine, neno linapotoka kinywani
mwa Mungu linakuwa na kila kinachohitajika ndani yake kufanikisha linalokisema
(fully equipped inside, with all it takes to fulfill what it talks about). Neno
linafanikiwa kwa sababu lina nguvu ya kutosha kutimiza kusudi lile lilotumwa
kulitimiza.
Mtu
anatakiwa awe na neno lililo na nguvu ndani yake yakumsaidia kufanikisha kile
anachohitaji ikiwamo kushinda vita dhidi ya shetani na mambo yake. Anahitaji
nguvu ya kumsaidi kuona anashika sheria ya Mungu, taratibu na amri za Mungu na
kuweka mfumo wa ufalme wa Mungu katika ya wanadamu. Hiyo nguvu inatoka ndani ya
neno la Mungu.
Mtu
haitaji neno tupu (mere word) bali lililo na nguvu ndani yake ili kuweza
kupigana vyema na kushinda vita dhidi ya shetani na mambo yake kisha kusimama
imara.
“Kwa hiyo vaeni silaha
zote za Mungu ili mweze kushindana siku ya uovu itakapokuja nanyi mkiisha
kufanya yote, simameni imara. Kwa hiyo simameni imara mkiwa mmejifunga kweli kiunoni…….. Vaeni chapeo
ya wokovu na mchukue upanga wa Roho, ambao ni Neno la Mungu” (Efeso
6:13-17)
Neno
la Mungu ni silaha, na kwenye mistari hii linatajwa likiwa na kazi mbili kuu,
kujilinda na kushambulia. Biblia inasema “…mmejifunga
kweli….” Kweli
ni neno la Mungu (Yoh 17:17). Na anaposema kiunoni anazungumzia habari ya
‘nafsi’ inayoundwa na fikra, mawazo na hisia. Nafsi ndiyo inayosaidia
kutengeneza msimama ndani ya mtu. Kwa kiyo anaposema “….mmejifunga kweli kiunoni…” alikuwa anamaanisha kuifunga nafsi
(fikra na mawazo) katika neno la Mungu. Nafsi ikubaliane na neno la Mungu. Hii
inamfanya mtu kuwa amesimama imara sehemu au uwanja sahihi kupigana. Neno la Mungu ni upanga kwa ajili ya
kushambulia adui. Kwa hiyo mtu anahiji neno la Mungu kwa ajili ya kumuimarisha
na kumlinda na kwa ajili ya kumshambulia adui awapo vitani. La zaidi ni kwamba
silaha zote zinazotajwa katika Efeso 6, ni silaha moja tu kwa ajili ya
kushambulia na kumpiga adui, nayo ni neno la Mungu. Nyingine zote ni kwa ajili ya
kujilinda (Protection)
Kwa
hiyo mtu anaongezeka kuwa hodari katika vita kwa kadiri anavyopata mda mwingi
wa kusoma, kusikiliza na kutafakari neno la Mungu kila siku. Neno linafyonzwa
kuingia rohoni mwa mtu kwa kutafakari hilo neno pamoja na Roho mtakatifu. Kazi
ya Roho Mtakatifu ni kukufunulia yaliyofichwa ndani ya kilo neno, na huwezi
kuyapata hayo isipokuwa wakati wa kutafakari hilo neno. Kwa kutafakari hilo
neno ndipo unapopata ufahamu sahihi wa kufanya mambo. Huwezi pia kufanya sawa
sawa na hilo neno isipokuwa umepata nafasi ya kutafakari hilo neno na kupata
ufahamu wa namna wa kulifanya na nguvu ya kulifanya sahihi.
“Kitabu hiki cha torati
kisiondoke kinywani mwako, Bali yatafakari
maneno yake mchana Na usiku, upate kuangalia kutenda sawa sawa Na maneno yote yaliyoandikwa humu; maana ndipo
utakapofanikisha njia yako, kisha ndipo utapapostawi sana” (Yoshua 1:8)
Kutafakari
neno, kunampa mtu ufahamu na nguvu ya kutenda sawa sawa na hilo neno na
kufanikisha njia yake. Ataendelea kustawi vizuri kwa kadiri anapopata mda
mwingi kutafakari hilo neno. Inapasa kuendelea na kutafakari hilo neno mpaka
anapopata ufunuo kwa kuvuviwa na Roho mtakatifu na anapoendelea kutumia ufahamu
huo anazidi kuimarika rohoni. Narudia tena, anapoendelea kuutumia (practice)
huo ufahamu. Yesu katika Marko 4:24 akiwa na watu,
“Akawaambia, angalieni msikialo; kipimo kile
mpimacho ndicho mtakachopimiwa, na tena mtazidishiwa” (Marko 4:24)
Kwa
tafsiri ya kiingereza (Amplied Bible) inasomeka hivi,
“And He said to them, Be
careful what you are hearing, The measure [of thought and study] you give [to
the truth you hear] will be the measure [of virtue and knowledge] that comes
back to you and more [besides] will be given to you who hear”
Kwa
tafsiri isiyo rasmi Ikiwa na maana “Akawaambia, angalieni msikialo, kipimo kile
(cha tafakari na kujifunza) mkipimacho kwa kweli muisikiayo, kitakuwa ndicho
kipimo cha (nguvu na maarifa) kitakachowajilia, na zaidi mtazidishiwa kwenu
ninyi mnaosikia”
Mtu
akitumia mda kidogo kutafakari atakuwa na ufahamu na nguvu kidogo, bali kwake
yeye anayetumia mda mwingi kutafari kwake yeye hupewa vingi. Na kweke yeye
asiyetaka kutafakari neno, anahesabiwa amekataa maarifa, kwake yeye maangamizo
ni hakika na BWANA humkataa yeye pamoja na watoto wake.
Biblia
inasema “Watu
wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa; kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa, mimi
name nitakukataa wewe, usiwe kuhani kwangu mimi; kwa kuwa umeisahau sheria ya
Mungu wako, mimi nami nitawasahau watoto wako” (Hosea 4:6)
Basi
neno la kristo na likae kwa wingi moyoni ili kuweza kufanikiwa.
Mungu
akubariki, andelea kufatilia mfululizo wa somo hili.
NAMNA YA KUKUZA NA KUIMARISHA ROHO YAKO-2
Reviewed by Unknown
on
6:34:00 PM
Rating:
No comments: